Nay Wa Mitego – Haki Lyrics
Haki Lyrics By Nay Wa Mitego
Haki haki haki haki
Haki haki haki haki
a$$alamu alaikum, ndugu zangu waislam, amen
Bwana asifiwe ndugu zangu wakristo, Amen
Mambo niaje yooh wanangu wa geo, woyoo
Na wapagani wote mnaamini mtaiona pepo
Haya ni wamitego tena nimerudi tena
Tega sikio ninamengi ya kusema
Sio CCM, Sio CUF, ACT wala CHADEMA
Wakiwauliza nani wajibu Ney Amesema
Usitangaze amani pasipokuwa na haki,
Penye haki, aman hutamalaki
Haki huinua taifa sio amani ya kinafki
Jana walituona tope, Leo tumekuwa almasi
Nawakumbusha polisi Jeshi la wananchi
Wanasiasa wasifanye mkawatesa wananchi
Hii nchi ya vyama vingi, na vyama vyote ni sawa
Chama chochote kinaweza kutawala